IQNA

Wakristo washirikiana na Waislamu Misri kukarabati msikiti

14:32 - August 27, 2021
Habari ID: 3474231
TEHRAN (IQNA)- Wanakijiji Wakristo wanashirikiana na Waislamu katika kukarabati msikiti mmoja wa kale katika mkoa wa Al Minya nchini Misri.

Kwa mujibu wa  taarifa, wakaazi wa kijiji kimoja mkoani Al Minya ambao ni Waislamu na Wakristo wote wameweka kazi zao kando na kushiriki katika ukarabati wa Msikiti wa Al-Amrawiambao ulijengwa karne kadhaa zilizopita.

Inadokezwa kuwa mkaazi mmoja wa kijiji hiyo ambaye ni Mkristo ndiye aliyetoa pendekezo la kwanza kukarabatiwa msikiti huo, na baada ya wakaazi  wote wa kijiji kuafiki ukarabati ulianza.

Misri ni nchi ya Kiislamu iliyo kaskazini mwa Afrika na idadi ya watu nchini humo inakadiriwa kuwa ni milioni 100. Zaidi ya asilimia 90 ya wakazi wa Misri ni Waislamu na waliosalia ni Wakristo. Watu wa Misri, wawe ni Waislamu au Wakristo wamekuwa wakiishi kwa amani na maelewano na husaidiana mara kwa mara katika masuala ya kidini.

مشارکت مسیحیان و مسلمانان در بازسازی مسجدی در مصر
 
مشارکت مسیحیان و مسلمانان در بازسازی مسجدی در مصر
 
مشارکت مسیحیان و مسلمانان در بازسازی مسجدی در مصر

3993022/

captcha