iqna

IQNA

iran
Mwezi wa Ramadhani na Diplomasia
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewapongeza viongozi na wananchi wa nchi za Kiislamu kwa mnasaba wa kuwadia mwezi mtukufu wa Ramadhani na kusema kuwa, ni wajibu wa viongozi wa nchi za Kiislamu kuhimiza na kudumisha amani na undugu baina ya Waislamu.
Habari ID: 3478497    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/12

Diplomasia ya Kiislamu
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza utayarifu wake wa kupanua uhusiano wa kiutamaduni kati ya Iran na Algeria kwa kuzingatia misikiti kama msingi na katika mwelekeo wa kuongeza maarifa, sayansi na kujenga umoja na mafungamano katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 3478444    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/03

Diplomasia
IQNA-Rais Seyed Ebrahim Raisi wa Iran amesisitiza kuwa, bara la Afrika lina nafasi muhimu katika sera za kigeni za serikali ya Iran na kuongeza kuwa: "Uhusiano na Afrika kwa ujumla na hasa nchi za Kiislamu barani Afrika una nafasi maalum sana katika sera zetu za kigeni."
Habari ID: 3478439    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/02

Siasa
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepiga kura yake katika dakika za awali za upigaji kura kwa ajili ya awamu ya 12 ya Majlisi ya Ushauuri ya Kiislamu (Bunge) na awamu ya 6 ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi.
Habari ID: 3478434    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/01

Uchaguzi wa Iran
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema: Maadui wa Iran ya Kiislamu wana hofu ya kushiriki kwa wingi kwa wananchi katika uchaguzi hapa nchini.
Habari ID: 3478428    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/28

Ukumbi wa Picha
IQNA- Sherehe za ufunguzi wa Mashindano ya 40 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimefanyika leo Alhamisi tarehe 5 Shaaban 1445 Hijria Qamaria sawa na 15 Februari 2024.
Habari ID: 3478358    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/15

Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Iran
IQNA - Jopo la majaji wa Mashindano ya 40 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran linajumuisha wataalamu wa Qur'ani kutoka taifa mwenyeji pamoja na nchi nyingine nane.
Habari ID: 3478354    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/15

Mashindano ya Qur'ani ya Iran
IQNA –Raundi ya mwisho ya toleo la 8 la mashindano ya kimataifa ya Qur'ani kwa wanafunzi wa shule za Kiislamu duniani itaanza mjini Tehran siku ya Alhamisi.
Habari ID: 3478351    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/14

Mapinduzi ya Kiislamu
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Ebrahim Raisi amesema: Jamhuri ya Kiislamu inaongoza mapambano dhidi ya ugaidi na kutetea haki za binadamu.
Habari ID: 3478335    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/11

Mapinduzi ya Kiislamu
IQNA-Mamilioni ya wananchi wa Iran wameshiriki katika maandamano ya kuadhimisha miaka 45 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu yaliyotokea mwaka 1979 kwa uongozi wa Imamu Ruhullah Khomeini (MA).
Habari ID: 3478334    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/11

Qur'ani Tukufu
IQNA - Maonyesho yanayoangazia kazi za sanaa za Qur'ani Tukufu na bidhaa husika kutoka Iran yamezinduliwa katika mji mkuu wa Thailand wa Bangkok.
Habari ID: 3478317    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/07

Mashindano ya Qur'ani Tukufu
IQNA - Wakati duru ya mwisho ya Mashindano ya 40 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran inakaribia, wakuu wa kamati za maandalizi ya tukio hilo la Qur'ani waliteuliwa.
Habari ID: 3478301    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/04

Harakati ya Qur'ani
IQNA - Wizara ya Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuzindua kituo cha tarjama au tarjuma ya Qur'ani Tukufu.
Habari ID: 3478275    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/30

Watetezi wa Palestina
IQNA-Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mashtaka ya Afrika Kusini dhidi ya mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza yanapongezwa na kusifiwa na watu wote wanaopigania uhuru na ukombozi.
Habari ID: 3478260    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/27

Diplomasia
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uhusiano wa Iran na Mali pamoja na nchi nyingine za Afrika si wa kisiasa na kidiplomasia tu, bali umejengeka katika msingi wa maslahi ya pande mbili na pande kadhaa.
Habari ID: 3478250    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/25

Mashindano ya Qur'ani
IQNA - Seyed Abolfazl Aqdadsi, kijana mhifadhi Qur'ani Tukufu kutoka Iran, anaiwakilisha nchi yake katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya Bangladesh.
Habari ID: 3478236    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/22

Makabiliano na Mabeberu
IQNA- Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuikamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama katika Bahari ya Oman.
Habari ID: 3478185    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11

Taazia
IQNA-Wananchi wa Iran leo Ijumaa wamefanya shughuli ya mazishi ya pamoja kwa wahanga wa miripuko miwili ya kigaidi iliyotokea Jumatano katika mji wa Kerman kusini mashariki mwa nchi huku kamanda wa ngazi ya juu wa Iran akiahidi kuwasaka magaidi popote walipo.
Habari ID: 3478151    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/05

Taazia
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe maalumu kufuatia kuuawa shahidi makumi ya wafanya ziara wa Shahid Qassem Soleimani na kusisitiza kuwa, wanaotenda jinai watambue kuwa wanamapambano wa njia ya Soleimani hawawezi kuhimili na kuvumilia jinai zao.
Habari ID: 3478142    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/04

Jinai ya Kigaidi
IQNA-Watu wasiopungua 94 wameuawa shahidi na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mashambulio mawili ya kigiadi katika mji wa Kerman kusini mashariki mwa Iran. Taarifa zinasema yamkini idadi ya waliofariki na majeruhi ikaongezeka.
Habari ID: 3478141    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/03