Mohammad Afzal ametumia uzoefu na umahiri wake wa kuandika kwa mbinu ya kaligrafia kuandika nakala moja ya Qur’ani kwa mkono.
Anasema kutokana na shughuli yake ya kuendesha taxi hakuwa anapata muda wa kuimarisha kipaji chake cha kaligrafia lakini baada ya kuanza zuio wakati huu wa corona alipata fursa ya kuandika Qur’ani. Anasema katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani alikuwa anatumia masaa 16-18 kuandika nakala yake ya Qur’ani.
Afzal anamshukuru baba yake ambaye ndiye alimfundisha kaligrafia. Mufti wa eneo hilo Sheikh Muhiuddin Faheem amesema ni vizuri kuwa Afzal alitumia muda wa zuio kwa njia ya busara.