Wawakilishi wa nchi 40 wanashiriki katika mashindano hayo ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Qur'ani na Sunnah ya Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu Libya.
Mashindano hayo ya kusoma na kuhifadhi Qur'ani yanafanyika kwa mara ya kwanza baada ya miaka 10 tokea nchi hiyo itumbukia katika vita vya ndani.
Libya ni nchi ya Kiislamu kaskazini mwa Afrika na ina karibu watu milioni moja waliohifadhi Qur'ani Tukufu kikamilifu.